Kigambera kilikuwa lugha ya Kiworrorran nchini Australia iliyozungumzwa na Wagambera katika jimbo la Australia Magharibi. Hakuna wasemaji ambao wamebaki kuongea lugha hii, yaani lugha ya Kigambera ilitoweka. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kigambera kiko katika kundi la Kiwunambal.