Mpeketoni


Mpeketoni
Nchi Kenya
Kaunti Lamu
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 25 000
Barabara ya Mpeketoni

Mpeketoni ni mji wa Kenya katika kaunti ya Lamu[1].

Si mji wa kale bali ulianzishwa katika miaka ya 1960 kama mradi wa kujenga makazi ya watu na rais wa jamhuri, Jomo Kenyatta.

Kwa asili eneo lilikaliwa na Wabajuni lakini wakati wa uhuru, na baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Wakenya wengi walirudi kutoka Tanzania hasa Wakikuyu, walio sehemu kubwa ya wakazi wa leo, pamoja na Waluo na Wakamba.

Mashamba yaliyoanzishwa na walowezi hao yanaendelea hadi leo. Kilimo ni hasa ya mahindi, pamba, muhogo, korosho, maembe, tikiti maji na ndizi.

Kabla ya ukoloni wa Kiingereza eneo lilikuwa chini ya usultani wa Zanzibar. Wafanyabiashara ya watumwa walitumia njia ya pwani kupeleka watumwa hadi Lamu. Hadi sasa mwembe mkubwa unakumbusha mahali ambako misafara ya watumwa ilipumzika na wafungwa walikula maembe na kuacha mbegu.

Karibu na Mpeketoni kuna ziwa Kenyatta.

Vijiji ndani ya tarafa ni pamoja na Kiongwe, Baharini, Mkunumbi, Bomani, Uziwa, Mapenya, Lakeside, Kibaoni.

  1. https://www.knbs.or.ke/?wpdmpro=2019-kenya-population-and-housing-census-volume-ii-distribution-of-population-by-administrative-units

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy