Waburunge

Barabara katika wilaya ya Kondoa linakopatikana kabila la Waburunge

Waburunge ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Dodoma, Wilaya ya Kondoa. Lugha yao ni Kiburunge, mojawapo ya lugha za Kikushi.

Waburunge kwa idadi ni wachache sana (300,000 hivi) na wanapatikana katika tarafa za Goima na Mondo, pia wachache wapo katika kata za Gwandi, Kondoa Mjini. Sasa hivi wanakaa kila kona ya Tanzania na wanapenda kushirikiana na watu wa makabila tofauti.

Lugha yao si ya Kibantu ila ina uhusiano kidogo na lugha za Wairaqw na Wagorowa kwani Mburunge anaweza kuelewa Mwiraq anachokiongea kutokana na maneno yao kuwa na mizizi ileile bali viambishi tofauti.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy