Wamalila

Wamalila ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi hasa katika Mkoa wa Mbeya, Wilaya ya Mbeya Vijijini, kata za Isuto, Ilembo, Iwiji, Masoko, Santilya, Iyunga Mapinduzi, bonde la Mbalizi na nyingine pia.

Lugha yao ni Kimalila, mojawapo ya lugha za Kibantu, ambayo inafanana sana na Kisafwa na Kinyiha kwa sarufi na maneno, na kutofautiana kwa baadhi ya matamshi na lafudhi.


From Wikipedia, the free encyclopedia ยท View on Wikipedia

Developed by Tubidy