Afeli

1. Sayari kwenye afeli yake 2. Sayari kwenye periheli yake 3. Jua

Afeli (kutoka Kiing. aphelion) ni mahali katika obiti ya sayari au magimba mengine ya angani ambako yako mbali zaidi na Jua. Jina linatokana na Kigiriki από "apo" (mbali) na Ήλιο "helio" (jua).

Kinyume chake ni periheli inayomaanisha sehemu ya njiamzingo iliyo karibu kabisa na jua.

Majina hayo hutumiwa kwa sababu obiti au njiamzingo ya Dunia si duara kamili, bali lina umbo la duaradufu. Yasingekuwa na maana kama njiamzingo ingekuwa duara kamili lakini hii haitokei hali halisi.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy