Agostino wa Hippo

Picha ya kale zaidi (karne ya 6) ya Agostino katika kanisa la Laterani, Roma (Italia).
Agostino wa Hippo akibatizwa na Ambrosi, mwaka 387.

Agostino wa Hippo (Thagaste, leo Souk Ahras nchini Algeria, 13 Novemba 354Hippo, leo Annaba, Algeria, 28 Agosti, 430) alikuwa mtawa, mwanateolojia, padri na hatimaye askofu mkuu wa Hippo.

Ndiye aliyekuwa kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki katika Afrika Kaskazini mwanzoni mwa karne ya 5.

Baada ya ujana uliovurugika kinadharia na kimaadili, aliongokea imani Katoliki, akabatizwa na Ambrosi huko Milano, Italia. Kisha kurudi Afrika Kaskazini, alishi kitawa na marafiki kadhaa, akimtumikia Mungu na kusoma Maandiko Matakatifu. Askofu kwa miaka 34, akilisha kundi lake kwa hotuba na maandishi mengi ambamo alifafanua kwa hekima imani sahihi na kupinga kwa nguvu aina mbalimbali za uzushi za wakati ule[1].

Kutokana na maisha, mafundisho na maandiko yake bora, tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu na babu wa Kanisa.

Mwaka 1298 Papa Bonifasi VIII alimuongezea sifa ya mwalimu wa Kanisa.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyoaga dunia[2].

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/24250
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy