Anga

Anga lenye mawingu.
Anga la mwezi ni jeusi; angani inaonekana dunia yetu. Kama dunia isingekuwa na angahewa kama mwezi rangi ya anga ingekuwa nyeusi pia.

Anga (mara nyingi pia: mbingu) ni uwazi ule mkubwa tunaoona juu yetu tukiinua kichwa nje ya jengo. Tukisimama kwenye tambarare au juu ya mlima kwenye mchana bila mawingu unaonekana kama nusutufe yenye rangi ya buluu. Ile buluu inaongezeka tukitazama juu zaidi kulingana na sehemu karibu na upeo. Wakati wa usiku anga ni jeusi lakini limejaa nuru za nyota.

Kwa lugha nyingine anga ni eneo la angahewa au upeo unaojaa hewa juu ya uso wa ardhi. Sehemu hiyo imejaa molekuli za gesi za angahewa hasa nitrojeni na oksijeni; ni molekuli hizo zinazoakisisha nuru ya jua na kusababisha rangi ya buluu ya anga wakati wa mchana. Bila hewa, anga lingekuwa jeusi muda wote jinsi lilivyo mwezini (linganisha picha).

Wakati wa mchana tunaona jua angani lisipofunikwa na mawingu. Wakati wa usiku tunaona mwezi na nyota zinazoonekana pia asubuhi na jioni ambako nuru ya jua haina nguvu bado au tena.

Mengine yanayoonekana angani ni mawingu, upinde wa mvua, ndege au eropleni.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy