Arusha (mji)


Jiji la Arusha
Mji wa Arusha na Mlima Meru
Mji wa Arusha na Mlima Meru
Mji wa Arusha na Mlima Meru
Mahali paJiji la Arusha
Mahali paJiji la Arusha
Jiji la Arusha is located in Tanzania
Jiji la Arusha
Jiji la Arusha
Majiranukta: 03°22′S 36°41′E / 3.367°S 36.683°E / -3.367; 36.683
Nchi Tanzania
Mkoa Arusha
Wilaya Arusha
Kata 25
Mitaa 155
Serikali[1]
 - Aina ya serikali Halmashauri ya Jiji
 - Mstahiki Meya Maximilian Matle Iranqe
 - Kaimu Mkurugenzi wa Jiji Hargeney Reginald Chitukuro
Eneo
 - Jumla 267 km²
Mwinuko 1,457 m (4,777 ft)
Idadi ya wakazi (2022)https://www.nbs.go.tz
 - Wakazi kwa ujumla 617,631
 - Mtawanyiko wa watu 1,560/km² (4,040.4/sq mi)
EAT (UTC+3)
Msimbo wa posta 231xx
Kodi ya simu 027
Tovuti:  Halmashauri ya Jiji la Arusha

Arusha ni jiji lililomo kaskazini mwa Tanzania na makao makuu ya Mkoa wa Arusha. Kiutawala eneo la jiji la Arusha ni sawa na eneo la Wilaya ya Arusha Mjini. Ina postikodi namba 23100.

Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 416,442.[2]: 26  Mwaka 2022 walihesabiwa 617,631 [3].

Mji huo upo kando ya Mlima Meru kwenye ncha ya mashariki mwa Bonde la Ufa na umezungukwa na baadhi ya mandhari maarufu barani Afrika zikiwa pamoja na mbuga za wanyama. Hifadhi ya Arusha, Hifadhi ya Wanyama ya Serengeti na Ngorongoro, Ziwa Manyara, Olduvai Gorge, Hifadhi ya Tarangire na mlima Kilimanjaro vipo karibu na mji huu.

Mji huu umezungukwa na milima kaskazini na mashariki, na mazingira yake ni mchanganyiko wa misitu ya savanna na misitu mabaki. Hali ya hewa ni nzuri sana.

Hadi sasa ni makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na za Mataifa.

  1. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; no text was provided for refs named ArushaCC
  2. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; no text was provided for refs named Sensa_2012
  3. https://www.nbs.go.tz

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy