Azerbaijan

Azərbaycan Respublikası
Jamhuri ya Azerbaijan
Bendera ya Azerbaijan Nembo ya Azerbaijan
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa:
Wimbo wa taifa: Azərbaycan Respublikasının Dövlət Himni
Lokeshen ya Azerbaijan
Mji mkuu Baku
40°22′ N 49°53′ E
Mji mkubwa nchini Baku
Lugha rasmi Kiazeri
Serikali Jamhuri
Ilham Aliyev (İlham Əliyev)
Ali Asadov (Əli Əsədov)
Uhuru
Ilitangazwa
Ilikamilishwa

30 Agosti 1991
25 Desemba 1991
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
86,600 km² (ya 112)
1.6
Idadi ya watu
 - 2019 kadirio
 - 1999 sensa
 - Msongamano wa watu
 
10,097,171[1] (ya 91)
7,953,438
115/km² (ya 99)
Fedha Manat (AZN)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+4)
(UTC+5)
Intaneti TLD .az
Kodi ya simu +994

-


Ramani ya Azerbaijan

Azerbaijan (pia: Azabajani, Azebajani) ni nchi ya Kaukazi kati ya Ulaya na Asia.

Imepakana na bahari ya Kaspi, Urusi, Georgia, Uturuki, Armenia na Uajemi.

Azerbaijan ni pia jina la mikoa miwili magharibi mwa Uajemi (Azerbaijan ya Mashariki na Azerbaijan ya Magharibi); nchini Uajemi takriban 16% za wakazi ni Waazeri; kwa jumla walioko Uajemi ni wengi kushinda walioko Azerbaijan yenyewe.

Eneo la Nakhichevan ni sehemu ya Azerbaijan inayopakana na Uturuki na Uajemi lakini imetenganika na sehemu kubwa ya nchi kwa sababu katikati kuna eneo la Armenia.

Eneo la Nagorno-Karabakh linalokaliwa na Waarmenia ndani ya Azerbaijan lilijitangaza nchi huru mwaka 1991 lakini haijatambuliwa na umma wa kimataifa.

Azerbaijan ni nchi mwanachama wa baraza la Ulaya tangu mwaka 2001. Hivyo kisiasa inahesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya, lakini kijiografia mara nyingi yahesabiwa kuwa sehemu ya Asia ya Magharibi.

  1. azadlıq saytı: demoqrafik vəziyyət – xəbərin yayınlanma tarixi: 11 iyun 2019

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy