Ceuta

Kisiwa cha Ceuta
Ceuta (Hispania)

Ceuta (tamka: the-uta; kwa Kiarabu: سبتة sabta) ni mji wa Kihispania kwenye pwani ya Mediteranea ambao upande wa bara unazungukwa na eneo la Moroko. Ceuta iko karibu na mji wa Tetouan upande wa Moroko. Umbali na Hispania ni km 21 kuvuka mlango wa bahari wa Gibraltar.

Pamoja na mji wa Melilla ni sehemu ya Hispania na Umoja wa Ulaya kisiasa , lakini kijiografia ni sehemu ya Afrika. Moroko inadai ni sehemu ya eneo lake la kitaifa.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy