Chai ni kinywaji kinachotengenezwa kwa kulowesha majani ya mchai (Camellia sinensis) katika maji ya moto. Wakati mwingine hata vinywaji vinavyopatikana kwa kutumia majani ya mimea mingine vinaitwa "chai".
Watu hunywa chai kwa sababu inatoa uchovu. Athari hii inatokana na dawa ya kafeini iliyopo ndani ya chai sawa na kahawa. Hapo awali, chai ilitumika kama bidhaa ya dawa. Matumizi yake kama kinywaji yalienea sana wakati wa Nasaba ya Tang ya China.