Chama cha Jubilee

Naibu Kiongozi wa Chama William Ruto (wa pili kushoto), Rais na Kiongozi wa Chama Uhuru Kenyatta (wa pili kulia), na Katibu Mkuu wa Chama cha Jubilee Raphael Tuju (kulia) .

Chama cha Jubilee cha Kenya ni chama cha kisiasa katika Jamhuri ya Kenya. Kilianzishwa mnamo 8 Septemba 2016, kufuatia kuunganishwa kwa vyama 11 vidogo.

Wakati wa uchaguzi wa 2017, Chama cha Jubilee kilipata viti vingi katika Bunge la Kenya na kiongozi wa chama hicho, Uhuru Kenyatta, alichaguliwa tena kuwa rais.

Tangu Januari 2019, chama hicho kimeonyesha dalili za kufarakana.

Chama cha Jubilee
Jina kamiliJubilee party
Jina la utani-
ImeanzishwaMachi 10, 2017 (2017-03-10)
MmilikiUhuru Kenyatta
MwenyekitiDavid Murathe

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy