Dioksidi kabonia

Dioksidi kabonia

Dioksidi kabonia (pia: dioxidi ya kaboni, pia kabonidayoksidi[1], hewa ukaa, gesi ya ukaa) ni kampaundi inayounganisha atomi mbili za oksijeni na atomi moja ya kaboni katika molekuli. Fomula yake ya kikemia ni CO2.

Katika mazingira ya kawaida hutokea kama gesi inayoganda kwenye halijoto chini ya -78.5°C. Katika hali ya gesi haina ladha wala harufu.

Dioksidi kabonia ina matumizi mbalimbali, kwa mfano kama gesi katika vinywaji aina za soda na bia, katika kizima moto za kupambana na moto penye umeme na mengine mengi.

Dioksidi kabonia inatokea wakati viumbehai wanapumua na kutoa pumzi; inatokea zaidi wakati wa kuchoma maada ogania yaani mada yenye kaboni ndani yake. Mimea inahitaji gesi hii kwa mchakato wa usanisinuru inamojenga chakula chao. Inabadilisha CO2 kuwa sukari aina za glukosi.

  1. dioksidi kabonia ni pendekeo la KAST, dioksidi ya kaboni ya TUKI-ESDD3, kabonidayoksaidi ya TUKI-KKS,

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy