Dola Takatifu la Kiroma

Dola Takatifu la Kiroma si sawa na Dola la Roma la Kale.
Ramani ya Dola Takatifu la Kiroma yaonyesha mikoa yake.
Maeneo ya Dola Takatifu la Kiroma pamoja na mipaka ya nchi za sasa.

Dola Takatifu la Kiroma (Kijerumani: Heiliges Römisches Reich, Kilatini: Sacrum Romanum Imperium) lilikuwa jina la Ujerumani kati ya takriban mwaka 1000 na 1806. Lakini dola hilo, licha ya Ujerumani, lilikuwa pia na maeneo makubwa, yakiwa ni pamoja na Austria, Italia ya Kaskazini, Ubelgiji, Uholanzi na Ucheki wa leo.

Mipaka yake yalibadilika mara kadhaa katika karne nyingi za kuwako kwake.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy