Dunia

Dunia
Dunia katika anga-nje, kama ilivyoonwa na wanaanga wa Apollo 17.
Dunia katika anga-nje, kama ilivyoonwa na wanaanga wa Apollo 17.
Jina
Asili ya jinaKar. دنيا, (dunyaa)
Majina mengine
Ardhi, nchi
Alama🜨
Tabia za njiamzingo
Umbali mfupikm 147,098,450
au 0.983292
Umbali mrefukm 152,097,597
au 1.01671
km 149,598,023
au 1.0
Uduaradufu0.0167086
siku 365.256363004
Mwinamo0.00005° toka njia ya Jua
MieziMwezi
Tabia za kimaumbile
km 6371.0
Tungamokg 5.972168×1024
g/cm3 5.5134
Uvutano wa usoni
m/s2 9.80665
siku 1.0
siku 0.99726968
Weupe0.306 (Bond)
0.367 (jiometri)
HalijotoK 287.91 (14.76°C)

Dunia ni violwa vya angani ambapo juu yake tunaishi sisi binadamu na viumbehai wengine wengi, tukipata mahitaji yetu, kuanzia hewa ya kutufaa na maji.

Dunia ni mojawapo ya sayari nane zinazozunguka Jua letu katika anga-nje. Kati ya sayari za Mfumo wa Jua, Dunia yetu ni sayari ya tatu kutoka kwa Jua.

Masafa baina yake na Jua ni kilomita milioni 150 au kizio astronomia 1. Dunia huchukua siku 365.256 kulizunguka Jua, na masaa 23.9345 kuuzunguka mhimili wake na upana wake ni kilomita 12,756.

Umri wa Dunia hukadiriwa kuwa miaka bilioni 4.5[1][2].

Ni mahali pekee katika ulimwengu panapojulikana kuna uhai ulioaminiwa kuanza miaka bilioni 3.5 iliyopita[3].

Uhai unapatikana kwa spishi milioni 10-14 za viumbe hai pamoja na wanadamu waliokadiriwa kuwa sasa bilioni 7.2[4].

  1. [http://sp.lyellcollection.org/content/190/1/205.abstract G. Brent Dalrymple: The age of the Earth in the twentieth century: a problem (mostly) solved, The Geological Society of London 2001]
  2. [http://www.talkorigins.org/faqs/faq-age-of-earth.html Chris Stassen, The Age of the Earth, (The Talk Origins Archive, 2005)
  3. Schopf, JW, Kudryavtsev, AB, Czaja, AD, and Tripathi, AB. (2007). Evidence of Archean life: Stromatolites and microfossils. Precambrian Research 158:141–155.
  4. http://www.worldometers.info/world-population/

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy