'
Eratosthenes | |
---|---|
Amezaliwa | 276 KK |
Amefariki | 194 KK |
Kazi yake | mtaalamu wa hisabati, jiografia |
Eratosthenes wa Kirene (kwa Kigiriki Ερατοσθένης ο Κυρηναίος; 276 KK - 194 KK) alikuwa mtaalamu wa hisabati, jiografia, historia na lugha tena mkurugenzi wa maktaba ya Aleksandria katika Misri. Anakumbukwa hasa kama mtu wa kwanza aliyekadiria mzingo wa dunia. Anasemekana aliibuni neno "jiografia".