Fedha

Fedha kwa maana ya malipo au sarafu angalia makala ya pesa

Fedha

Fedha (kutoka Kiarabu فضة fiddtan) ni elementi na metali yenye kifupi cha Ag (kutoka Kilatini: argentum) na namba atomia 47 katika mfumo radidia. Uzani atomia ni 107.86. Fedha huyeyuka kwa 1234.93 K (961.78°C) na kuchemka kwa 2435 K (2162°C).

Kiasili yatokea kama metali nyeupenyeupe na laini au kama mchanganyiko katika madini. Kati ya metali zote fedha ni wayaikaji na inapitisha vizuri umeme.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy