Filamu

Mcheza filamu za kuchekesha Chaplin
Alama mojawapo ya Filamu
Mwandaaji wa filamu nchini Tanzania

Filamu (kutoka Kiingereza film, pia movie au motion pictures) ni mfululizo wa picha zinazoonyesha mwendo wa watu au vitu na kuonekana na watazamaji kwenye skrini.

Ni aina ya mawasiliano yanayotumiwa kutolea hadithi au kuwaelezea watu kuhusiana na kujifunza fikra au mitazamo mipya katika jamii.

Watu katika kila pembe ya dunia huwa wanaangalia filamu ambazo zinaelezea hadithi fulani ikiwa kama kiburudisho, au njia ya mojawapo ya upenzi.

Filamu nyingi zinatengenezwa ili kuonyeshwa katika makumbi makubwa ya video au sinema.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy