Haki za watoto

Haki za watoto ni kimoja kati ya vifungu vya haki za binadamu[1] ambacho kinalenga hasa watoto[2].

Mapatano ya kimataifa juu ya Haki za Watoto yamekubaliwa na wanachama wa Umoja wa Mataifa. Watoto wanafafanuliwa kuwa "mtu yeyote mwenye umri chini ya miaka kumi na nane"[3].

Haki za watoto zinajumuisha haki ya kushirikiana na wazazi wote wawili, kutambuliwa kibinadamu na mahitaji ya msingi ya ulinzi wa mwili, chakula, elimu, huduma ya afya, na sheria zinazofaa kwa ukuaji wa mtoto, haki za kiraia za mtoto, uhuru wa kutokubaguliwa kutokana na rangi, jinsia, asili ya kitaifa, ulemavu, dini, kabila au sifa nyingine. Vile vile tafsiri ya haki za watoto zinalenga zaidi kuwapa watoto kuwa huru kimwili, kiakili na kimihemko kutokana na dhuluma na unyanyasaji. tafsiri nyingine ni pamoja na malezi na utunzaji wa mtoto.

"Haki za vijana" (Kiing. Youth Rights) zinajadiliwa pekee lakini hakuna mapatano ya kimataifa.

  1. https://www.un.org/en/about-us/universal-declaration-of-human-rights
  2. https://www.hrw.org/topic/childrens-rights
  3. Convention on the Rights of the Child, G.A. res. 44/25, annex, 44 U.N. GAOR Supp. (No. 49) at 167, U.N. Doc. A/44/49 (1989), entered into force Sept. 2 1990

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy