Imamu

Imamu akiongoza swala huko Kairo, Misri, mnamo 1865. Taswira ya Jean-Léon Gérôme.

Imamu (kutoka Kiarabu: إمام‎ imām) ni istilahi ya Kiarabu yenye maana mbalimbali. Mara nyingi inamtaja kiongozi wa Kiislam, kama kiongozi wa msikiti au wa jamii. Maana ya msingi ni yule anayetoa mwongozo akistahili kufuatwa; kwa maana isiyo ya kidini neno hili linaweza kutaja pia timazi au kamba inayotumiwa kuelekeza mwendo wa matofali wakati wa kujenga nyumba au ukuta.[1]

Imamu anaitwa yule anayeongoza sala wakati wa swala ya Kiislamu.

  1. [https://archive.org/details/LANESARABICENGLISHLEXICONDIGITIZEDTEXTVERSION Lane, Edward William: Arabic – English Lexicon], Perseus Collection Arabic Materials, Attribution-ShareAlike 3.0 United States - CREATIVE COMMONS, Online Version, Released Digitized Text Version v1.1, Kitabu cha kwanza uk. 90-92

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy