John Wesley

John Wesley

John Wesley (17031791) alikuwa mmoja wa waanzilishi wa kanisa la Kimethodisti. Alikuwa mchungaji wa Kianglikana na mwanatheolojia. Alikuwa kati ya viongozi wa kwanza katika harakati ya Wamethodisti.

Maisha ya Wesley yalikuwa na awamu tatu tofauti: ya kwanza katika Chuo Kikuu cha Oxford kwa kuanzisha "Klabu takatifu" (Holy Club), ya pili huku Wesley akiwa mmisionari huko Savannah, Georgia; na ya tatu baada ya Wesley kurudi Uingereza. Katika maisha yake yote, Wesley aliendelea kuwa Mkristo na mtumishi wa Kanisa la Uingereza, yaani Anglikana. Aliona kuwa harakati yake ilikuwa ndani ya mipaka ya Kanisa Anglikana[1], ingawa iliendelea kwa kuwa kanisa la pekee.

  1. Thorsen, Don (2005). The Wesleyan Quadrilateral. Emeth Press. uk. 97. ISBN 0-9755435-3-9.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy