Kalenda ya Ethiopia

Kalenda ya Ethiopia (kwa Kiamhari: የኢትዮጵያ ዘመን አቆጣጠር ye'Ityoṗṗya zemen aḳoṭaṭer) ni kalenda rasmi nchini Ethiopia na pia kalenda inayotumiwa na Wakristo walio wengi nchini Eritrea. Asili yake ni kalenda ya Wakopti kwa sababu Kanisa la Ethiopia kwa karne nyingi lilikuwa kama tawi la kanisa la Kikopti la Misri.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy