Kanisa la Kitume la Armenia

Ubatizo wa mfalme Tiridate III ulioingiza taifa la Armenia katika Ukristo.

Kanisa la Kitume la Armenia (kwa Kiarmenia: Հայ Առաքելական Եկեղեցի), ambalo pengine linaitwa pia Kanisa la Kiorthodoksi la Armenia au Kanisa la Kigregori, ni Kanisa la kitaifa la kale zaidi duniani (301).

Wafuasi wake wanahesabiwa kati ya Waorthodoksi wa Mashariki kwa sababu hawakubali Mtaguso wa Kalsedonia na Mitaguso ya kiekumeni iliyofuata.

Upande wa ibada, linatumia liturujia ya Armenia.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy