Kaskazini

Alama za dira zikionyesha kaskazini katika hali ya mkoozo

Kaskazini ni moja kati ya mielekeo minne mikuu ya dira. Mwelekeo wake ni ncha ya kaskazini ya dunia. Kinyume chake ni kusini.

Jina "kaskazini" limetokana na neno la Kiarabu "قيظ qiz" joto na "قيظ قائظ qiz qaez" hali ya hewa lenye joto sana; kutoka sehemu za Zanzibar au Uswahilini kwenda kaskazini kuelekea Somalia joto linaongezeka sana; upepo wa joto latokea huko.

Kaskazini kawaida huwa juu zaidi kwenye ramani. Kanada ipo kaskazini mwa nchi ya Marekani, Venezuela ipo kaskazini mwa nchi ya Brazil, na Urusi ipo kaskazini mwa nchi ya India. Ncha ya kaskazini ni kaskazini ya mbali unayoweza kwenda.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy