Kinyama-bapa | ||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Trichoplax adhaerens chini ya hadubini
| ||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||
| ||||||||
Ngazi za chini | ||||||||
Jenasi 3, spishi 3:
|
Vinyama-bapa ni aina za msingi za viumbehai vya bahari (visivyo vimelea) vyenye seli nyingi. Wana muundo sahili sana wa wanyama wote. Kufikia sasa, jenasi tatu, kila moja na spishi moja, zimepatikana: Trichoplax adhaerens, Hoilungia hongkongensis na Polyplacotoma mediterranea, ambapo ile ya mwisho huonekana msingi zaidi. Mbili za mwisho zimepatikana tu tangu 2017. Ingawa spishi ya kwanza iligunduliwa mnamo 1883 na mwanazoolojia wa Ujerumani Franz Eilhard Schulze (1840-1921) na tangu miaka ya 1970 ilichambuliwa zaidi na mtaalamu wa protozoolojia wa Ujerumani Karl Gottlieb Grell (1912-1994), jina la kawaida bado halipo kwa faila hii katika takriban lugha zote.