Kiswahili

Maeneo yenye wasemaji wa Kiswahili.
Mfano wa kusema Kiswahili.

Kiswahili ni lugha ya Kibantu yenye misamiati mingi ya Kiarabu (35%[1]), lakini sasa ya Kiingereza pia (10%), inayozungumzwa katika eneo kubwa la Afrika ya Mashariki.

Lugha hii ina utajiri mkubwa wa misamiati, misemo, methali, mashairi, mafumbo, vitendawili na nyimbo. Kiswahili hutumika kufundishia shuleni na kuna vitabu vingi vilivyotungwa kwa kutumia lugha hiyo, vikiwa pamoja na vile vya hadithi, hekaya au riwaya.

  1. "BBC - Languages - Swahili - A Guide to Swahili - 10 facts about the Swahili language". www.bbc.co.uk (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2022-05-17.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy