Kleri

Wakleri watatu: askofu mkuu Carey wa Kanisa Anglikana, Rabbi Sacks wa Umoja wa Masinagogi ya Jumuiya ya Madola, mufti mkuu Ceric wa Bosnia, wakiwa pamoja na J. Wallis, mhariri wa gazeti la Kiinjili "Sojournes", Marekani.
Daraja takatifu tatu za Kanisa la Kiorthodoksi zinavyojitokeza katika liturujia ya Kimungu: askofu (kulia, kwenye altare, nyuma ya ukuta wa picha), padri (kushoto), na mashemasi wawili (waliovaa rangi ya dhahabu).
Wakleri Waorthodoksi wa Ethiopia wakiongoza maandamano ya Mt. Mikaeli Malaika Mkuu.

Kleri ni kundi la watu wanaoongoza dini fulani. Jina linatokana na neno la Kigiriki "κλῆρος" - klēros, "bahati", "sudi" au also "urithi".

Katika madhehebu mengi ya Ukristo kleri ina daraja takatifu tatu: kuanzia juu ni uaskofu, upadri na ushemasi. Hata hivyo baadhi yao wanapewa pia majina mengine kulingana na huduma zao, kwa mfano: Papa, kardinali, monsinyori, abati, kanoni, arkimandrita n.k.

Katika Uislamu hakuna ukuhani, hivyo uongozi unategemea tu elimu ya dini: kuna mufti, imamu, ustadhi n.k.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy