Kusini

Alama za dira zikionyesha kusini katika hali ya mkoozo

Kusini ni moja kati ya mielekeo minne mikuu ya dira. Mwelekeo wake ni ncha ya kusini ya dunia. Kinyume chake ni kaskazini.

Jina "kusini" laaminiwa limetokana na neno lenye asili ya Misri ya Kale kwa ajili ya nchi ya Kushi iliyokuwepo upande wa kusini wa Misri katika Nubia (au Sudani ya leo) pamoja na Uarabuni ya Kusini. Jina la Kushi lapatikana pia katika masimulizi ya Biblia likimtaja mmoja wa wana wa Hamu katika kitabu cha Mwanzo 10:16 kama baba wa watu wa Kushi. Hili neno lilitumiwa na mabaharia Waarabu pia kutaja mwelekeo wa kusini na kwa umbo la "kusi" hasa upepo wa kusini. [1]

Ukitazama jua linapochomoza kusini huwa ni upande wa kulia. Kusini kawaida huwa chini zaidi kwenye ramani. Marekani ipo kusini mwa nchi ya Kanada, Tanzania ipo kusini mwa nchi ya Kenya, na Msumbiji ipo kusini mwa nchi ya Tanzania. Ncha ya kusini ni kusini ya mbali unayoweza kwenda.

  1. linganisha maelezo katika makala "kusini" katika kamusi ya M-J SSE

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy