Lagos

Lagos inavyoonekana kutoka bandari yake

Lagos ni mji mkubwa wa Nigeria. Ilikuwa mji mkuu wa nchi hadi mwaka 1991.

Ikiwa na wakazi takriban milioni 12 katika eneo la jiji na milioni 15 - 22 katika rundiko la mji ni kati ya miji mikubwa zaidi ya Afrika; inawezekana kwamba idadi ya watu imeshapita ya Kairo, hivyo kuwa jiji lenye watu wengi barani Afrika[1].

Lagos ilianzishwa kama mji wa bandari uliokua juu ya visiwa vidogo karibu na mdomo wa wangwa wa Lagos unapounganika na Bahari ya Atlantiki.

Bandari ya Lagos iko kati ya bandari muhimu zaidi Afrika[2][3].

  1. linganisha worldpopulationreview.com inayorejea taarifa ya New York Times ya 2012; ilitazamiwa 23 Novemba 2016
  2. "Africa's biggest shipping ports", Businesstech. 8 March 2015. iliangaliwa 23 Novemba 2016
  3. "Africa's top 10 ports", arabianbusiness 12 Mei 2008, iliangaliwa 23 Novemba 2016

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy