Lugha ya taifa

Lugha ya taifa ni lugha au lahaja iliyoteuliwa miongoni mwa zile zilizopo katika taifa fulani ili itumike katika mawasiliano ya jamii hiyo. Mara nyingi lugha ya taifa huteuliwa ili kukidhi haja ya mawasiliano miongoni mwa jamii.

Lugha ya taifa inakuwa kama kitambulisho cha taifa husika, kwa mfano, lugha ya Kiswahili nchini Tanzania inakuwa kama nembo ya taifa, kwa sababu ni sehemu ya utamaduni yaani mila na desturi za Watanzania.

Dhana ya lugha ya taifa imetumika kwa namna tofauti katika mataifa tofautitofauti. Kwa kawaida lugha ya taifa ni lugha kuu, yaani lugha inayotumika katika shughuli za mahakama na siasa, katika ngazi ya taifa, kwa mfano, nchini Uingereza lugha kuu ni Kiingereza lakini Kiwelisi kina nafasi yake haswa katika eneo la Wales.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy