Lugha za Kihindi-Kiulaya

Uenezi wa lugha za Kihindi-Kiulaya (kijani cheupe) kati ya jamii za lugha nyingine duniani.
Uenezi wa wasemaji wa Kihindi-Kiulaya asilia kufuatana na nadharia ya Kurgan
Uenezi katikati ya milenia ya 3 KK
Uenezi katikati ya milenia ya 2 KK
Uenezi takriban mwaka 250 KK

Lugha za Kihindi-Kiulaya ni jamii ya lugha iliyo kubwa kuliko zote duniani. Imekadiriwa kuna lugha hai 445 za jamii hiyo na wasemaji bilioni 3.2 katika mabara yote (46% za watu wote wa leo).

Uenezi huo umetokana hasa na historia ya ukoloni wa Kizungu uliopeleka lugha za Ulaya pande zote za dunia.

Lugha zenye wasemaji zaidi ya milioni 100 ni: Kihispania, Kiingereza, Kihindustani (Kihindi/Kiurdu), Kireno, Kibengali, Kipanjabi na Kirusi.

Nyingine zenye wasemaji zaidi ya milioni 50 ni: Kijerumani, Kifaransa, Kimarathi, Kiitalia na Kiajemi.

Lugha za Kihindi-Kiulaya

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy