Lugha za Kirumi

Lugha za Kirumi duniani:
buluuKifaransa; kijaniKihispania; machungwaKireno; njanoKiitalia; nyekunduKiromania

Lugha za Kirumi ni lugha zilizotokana na Kilatini kilichokuwa moja kati ya lugha za kale za Kihindi-Kiulaya.

Ni lugha mama kwa watu milioni 800 hivi duniani.

Zimehesabiwa hadi lugha 23 za namna hiyo, ingawa baadhi kwa wengine ni lahaja tu. Tena kuna Krioli nyingi zenye asili katika lugha hizo. Kati ya Krioli hizo, ile ya Haiti na ile ya Shelisheli ni lugha rasmi nchini.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy