Maangamizi makuu dhidi ya Wayahudi wa Ulaya (kwa Kiingereza/Kigiriki: Holocaust, kwa Kiebrania Shoah השואה) yalikuwa mauaji ya Wayahudi milioni 5-6 wa Ulaya wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia kati ya miaka 1940 na 1945. Mauaji hayo yalipangwa na kutekelezwa na serikali ya Ujerumani chini ya Adolf Hitler kwa msaada wa serikali za nchi zilizofungamana na Ujerumani au zilizokuwa chini ya jeshi la Ujerumani.
Mauaji hayo yalitekelezwa kwa njia ya