Mahindi

Masuke ya aina mbalimbali za mahindi.

Mahindi ni mbegu za mmea wenye asili ya Amerika ambao unaitwa mhindi na chakula muhimu cha watu katika pande nyingi za dunia.

Ni nafaka yenye wanga na katika Afrika ya Mashariki huliwa hasa kama ugali. Ugali unatengenezwa kwa kutumia unga wa mahindi.

Mahindi mabichi yasiyokauka huliwa pia kwa kubanika suke lote juu ya moto.

Mahindi yaliyosagwa hutumiwa pia kwa kutengeneza pombe ya kienyeji.


From Wikipedia, the free encyclopedia ยท View on Wikipedia

Developed by Tubidy