Mamalia

Mammalia
Kangaruu ni mamalia wa Australia
Kangaruu ni mamalia wa Australia
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Faila: Chordata
Ngeli: Mammalia
Ngazi za chini

Mamalia ni wanyama ambao wanawanyonyesha watoto wao maziwa kwa kutumia viwele vyao.

Wana damu moto na kupumua kwa mapafu.

Kuna takriban spishi 5,400 za mamalia. Spishi 5 kati ya hizo wanataga mayai, lakini wengine wote wanazaa watoto hai.

Ukubwa unatofautiana sana, kuanzia spishi ndogo aina ya popo mwenye urefu wa sentimita 4 pekee hadi spishi kubwa nyangumi buluu mwenye urefu wa mita 33.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy