Melanesia

Mahali pa Melanesia katika Pasifiki kaskazini ya Australia
Mwenyeji wa Vanuatu awafundisha watoto kutengeneza moto

Melanesia ni eneo la Bahari ya Pasifiki lililoko kaskazini kwa Australia. Ni mojawapo kati ya makundi makubwa matatu ya visiwa vya Pasifiki pamoja na Mikronesia na Polynesia.

Jina lake limeundwa na maneno ya Kigiriki μέλας cheusi na νῆσος kisiwa yaani "visiwa vyeusi" au zaidi "Visiwa vya Weusi". Nahodha Mfaransa Jules Dumont d'Urville alitunga jina hilo mwaka 1832 akitaka kutaja wazawa waliokuwa na rangi nyeusi-nyeusi.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy