Melilla

Kisiwa cha Melilla
Ramani ya mji wa Melilla

Melilla (tamka: me-li-ya; kwa Kiarabu: مليلية, Meliliya; jina rasmi: Ciudad Autónoma de Melilla = Mji wa kujitawala wa Melilla) ni mji wa Hispania kwenye pwani ya Mediteranea unaozungukwa na eneo la Moroko upande wa bara. Umbali na Hispania bara ni takriban km 170 kuvuka bahari. Mji ulio karibu upande wa Moroko ni Nador kwenye umbali wa km 15.

Pamoja na mji wa Ceuta kisiasa ni sehemu ya Hispania na Umoja wa Ulaya, kijiografia ni sehemu ya Afrika. Moroko inadai ni sehemu ya eneo lake la kitaifa.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy