Mfumo wa chama kimoja

Aina za serikali duniani
*Nyekundu - Serikali ya kiraisi
*Kijani - Serikali ya raisi pamoja na athira kubwa ya bunge
*Kijani-kizeituni - Serikali ya kiraisi pamoja na waziri mkuu
*Machungwa - Serikali ya kibunge
*Kahawiya - Jamhuri zinazoruhusu chama kimoja pekee
Mengine: Ufalme au serikali ya kijeshi
Angalizi nchi mbalimbali zinazojiita "jamhuri" hutazamiwa na wengine kama udikteta. Ramani ianonyesha hali ya kisheria si hali halisi.

Mfumo wa chama kimoja ni utaratibu wa kisiasa unaoruhusu chama cha kisiasa kimoja tu.

Mara nyingi mfumo huo umeanzishwa kwa kupiga marufuku vyama vyote vingine. Kuna pia nchi ambako vyama mbalimbali viko, lakini havina nafasi ya kushiriki katika uchaguzi au vinazuiwa kushindana na chama tawala.

Kihistoria mifumo hii ilitokea katika mazingira ya Ukomunisti, Ujamaa au Ufashisti. Mfumo huu ni karibu na udikteta.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy