Mifugo

Mchungaji na mifugo yake
Mifugo aina ya ng'ombe

Mifugo au Wanyama wa kufugwa ni wanyama wanaopatikana kutokana na ufugaji wa kibinadamu.

Wako tofauti na wanyamapori baada ya na mchakato mrefu ambako wanyama wa pori ama walijiunga na binadamu au walishikwa nao na watoto wao kuteuliwa kutokana na tabia zilizopendelewa na wafugaji wao. Tabia hizo ni pamoja na upole na uwezo wa kupatana na binadamu, uwezo wa kuzalisha kiasi fulani cha nyama au maziwa, uwezo wa kustawi kwa chakula fulani au katika mazingira mbalimbali.

Katika mchakato wa vizazi vingi tabia zilizolengwa ziliimarishwa katika spishi zinazofugwa.

Uteuzi huu umesababisha tofauti za kimaumbile na tofauti za tabia baina ya wanyama wa kufugwa na wanyamapori wa spishi ileile. Tofauti hizi zinaonekana katika rangi, ukubwa wa mwili, uwezo wa kuwasiliana na binadamu na mengine.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy