Milki ya Osmani

Milki ya Osmani mwaka 1683.
Sultani Mehmed Fatih aliyeteka Konstantinopoli mwaka 1453.

Milki ya Osmani (pia: Ottomani)[1] ilikuwa dola kubwa lililotawala upande wa mashariki wa Bahari Mediteranea pamoja na nchi nyingi za Mashariki ya Kati kati ya karne ya 14 na mwaka 1922.

Milki ilianzishwa na Waturuki Waosmani ikachukua nafasi ya ukhalifa wa Waabbasi na Milki ya Bizanti.

Mji wake mkuu ulikuwa Konstantinopoli (leo: Istanbul) na mtawala wake mkuu alikuwa Sultani wa Waosmani. Imani rasmi ya milki ilikuwa Uislamu hata kama katika maeneo mengi idadi kubwa ya wakazi walikuwa Wakristo.

Tabaka la viongozi wa kisiasa na wa kijeshi walikuwa Waosmani waliokuwa Waturuki pamoja na mchanganyiko wa Waislamu kutoka sehemu zote za milki yao, hasa Balkani. Kwenye uwanja wa uchumi na utawala Waosmani walitumia sana Wakristo Wagiriki na Waarmenia kutokana na elimu yao.

  1. Historia Kuu ya Afrika hutumia "Ottomani", umbo linalotokana na matamshi ya Kiingereza ya jina "عثمان", "uthman", labda pia kwa kukosea herufi za Kiarabu "ث th" na " t"; kwa hiyo kumtamka mwanzilishi "Otman"; katika lugha za Kifarsi na Kituruki herufi ya "ث th" ina matamshi ya "s", hivyo "Osmani".

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy