Mji mkuu

Dodoma, mji mkuu wa Tanzania.
Nairobi, mji mkuu wa Kenya.

Mji mkuu kwa kawaida ni mji wenye makao makuu ya serikali ya nchi fulani. Katika nchi nyingi mji huo ni pia mji mkubwa na muhimu zaidi kushinda miji mingine nchini. Huo ni sehemu yenye maendeleo makubwa sana katika nchi yoyote: ina kila huduma muhimu na miundombinu iliyo bora. Mfano: nchini Tanzania mji mkubwa ni Dar es Salaam, ingawa makao makuu ni Dodoma.

Kuna nchi ambako mji mmoja umeteuliwa kuwa mji mkuu katika katiba au kwa sheria fulani. Kumbe kuna nchi nyingine ambako hakuna sheria yoyote lakini makao makuu yanaeleweka yapo mji fulani.

Nchi kadhaa zimeteua mji fulani kuwa mji mkuu kwa shabaha ya kubadilisha mwendo wa nchi au kama jaribio la kusahihisha historia yake.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy