Mkoa wa Manyara

Mkoa wa Manyara katika Tanzania
Wilaya za Mkoa wa Manyara

Mkoa wa Manyara ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 27000. Umepakana na mikoa ya Arusha na Kilimanjaro upande wa kaskazini, Mkoa wa Tanga upande wa mashariki, Mkoa wa Dodoma upande wa kusini na mikoa ya Singida na Shinyanga upande wa magharibi.

Mkoa wa Manyara umetengwa na Mkoa wa Arusha mwaka 2002 kwa azimio la rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiwa na eneo la km² 46,359.

Babati ndiyo makao makuu ya mkoa.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy