Mkoa wa Mara


Mkoa wa Mara
Mahali paMkoa wa Mara
Mahali paMkoa wa Mara
Mahali pa Mkoa wa Mara katika Tanzania
Majiranukta: 1°33′S 34°1′E / 1.550°S 34.017°E / -1.550; 34.017
Nchi Tanzania
Wilaya 7
Mji mkuu Musoma
Serikali
 - Mkuu wa Mkoa Mh. Kanali Enos Mfuru
Eneo
 - Jumla 30,150 km²
 - Maji 7,500 km² 
Idadi ya wakazi (2022)
 - Wakazi kwa ujumla 2,372,015
Tovuti:  http://www.mara.go.tz/

Mkoa wa Mara ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 31000.[1].

Umepakana na mikoa jirani ya Mwanza na Shinyanga upande wa kusini, Arusha upande wa kusini-mashariki, Kagera kwa njia ya Ziwa Nyanza (au Viktoria) na Kenya upande wa mashariki.

Jina linatokana na lile la mto Mara.

Musoma ndio makao makuu ya mkoa.

Idadi ya wakazi ilikuwa 2,372,015 wakati wa sensa ya mwaka 2022[2], kutoka 1,743,830 wa sensa ya mwaka 2012 [3], na 1,368,602 wa sensa ya 2002[4].

Kuna wilaya 9 zifuatazo katika mkoa wa Mara: Bunda Mjini, Bunda Vijijini, Serengeti, Tarime Vijijini, Tarime Mjini, Rorya, Butiama, Musoma mjini na Musoma vijijini.

Sehemu kubwa ya Hifadhi ya Wanyama ya Serengeti iko ndani ya Mkoa wa Mara.

  1. https://sw.wikipedia.orgview_html.php?sq=Albert Einstein&lang=sw&q=Mfumo_wa_Msimbo_wa_Posta_Tanzania
  2. https://www.nbs.go.tz
  3. Sensa ya 2012, Mara Region
  4. "Mara Region Homepage for the 2002 Tanzania National Census". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2003-12-15. Iliwekwa mnamo 2003-12-15.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy