Mkoa wa Singida

Mahali pa Mkoa wa Singida katika Tanzania.

Mkoa wa Singida ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania: mkoa huo upo kanda ya kati, ukipakana na mikoa ya Manyara upande wa kaskazini, Dodoma mashariki, Iringa na Mbeya kusini, Tabora upande wa magharibi na Shinyanga.

msimbo wa posta ni 43000.

Kuna wilaya saba za Iramba, Manyoni, Singida Vijijini na Singida Mjini, Ikungi, Itigi na Mkalama.

Katika sensa ya mwaka 2022 walihesabiwa wakazi 2,008,058 [1]. kutoka 1,370,637 wa mwaka 2012[2].

Wakazi wa wilaya za Singida mjini na kijijini ni hasa Wanyaturu. Walio wengi Iramba ndio Wanyiramba na wakiwa Wagogo wengi huko Manyoni. Pia kati ya wenyeji kuna Wanyisanzu na makabila mengine madogo. Makabila hayo wanaishi kwa amani na upendo.

Lugha kuu ni Kiswahili, lakini pia kila kabila wanaongea yao.

  1. https://www.nbs.go.tz
  2. Sensa ya 2012, Singida

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy