Mofimu

Mofimu ni kipashio kidogo kuliko vyote katika lugha chenye maana ya kisarufi /kileksika. Mofimu katika sarufi ni jina la sehemu ndogo kabisa yenye kuwakilisha maana katika neno. Kipashio hiki hakiwezi kuvunjwavunjwa zaidi bila kupoteza maana. Mfano:

  • "Analima" - A-na-lim-a

Neno analima lina mofimu nne ambazo hufungamana na kujenga neno analima. Kila moja ya mofimu hizi isimamapo pekee haina maana yoyote isipokuwa ina maana kisarufi ambayo humwezesha mwanaisimu kuchambua maana hiyo.[1]

  1. J.A. Masebo na Nyambari Nyangwine 2012, "Jitayarishe kwa Kiswahili", "Chapa ya Pili" - ISBN 978 9987 09 017 4

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy