Mungu ibariki Afrika

Noti za muziki wa nyimbo
Enock Sentonga,mtunzi wa wimbo wa Nkosi Sikeleli Afrika

Mungu Ibariki Afrika ni wimbo wa taifa wa Tanzania. Jina linatokana na maneno yake ya kwanza.

Asili yake ni wimbo Nkosi Sikelel' iAfrika wa Afrika Kusini. Enoch Sontonga ndiye mtunzi wake mwaka 1897.

Sehemu ya wimbo huu inatumika pia katika nyimbo za taifa za Afrika Kusini na Zambia. Huko nyuma ulitumiwa kama wimbo wa taifa wa Zimbabwe.

Mungu ibariki Afrika

Mungu ibariki Afrika
Wabariki viongozi wake
Hekima, Umoja na Amani
Hizi ni ngao zetu
Afrika na watu wake

KIITIKIO:

Ibariki Afrika
Ibariki Afrika
Tubariki watoto wa Afrika
Mungu ibariki Tanzania
Dumisha Uhuru na Umoja
Wake kwa Waume na Watoto
Mungu ibariki Tanzania na watu wake

KIITIKIO:

Ibariki Tanzania
Ibariki Tanzania
Tubariki watoto wa Tanzania

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy