Mzee

Padri wa Kiorthodoksi, Mtskheta, Georgia.

Mzee ni mtu aliyeishi miaka mingi baada ya kuzaliwa.

Katika jamii za Kiafrika, sawa na jamii nyingi duniani, neno "mzee" linatumiwa pia kama cheo cha heshima kwa kumtaja mtu mwenye mamlaka fulani.

Hapo kuna hoja ya kuwa mtu aliyeendelea katika umri anawazidi vijana kwa hekima na maarifa pia, kwa hiyo anafaa kutawala au kufanya maazimio au angalau kutoa ushauri.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy