Ngano

Kwa aina ya fasihi simulizi tazama makala ya Ngano (hadithi)

Ngano
(Triticum L.)
Ngano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Planta (mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Monocots (Mimea ambayo mche wao una jani moja tu)
(bila tabaka): Commelinids (Mimea kama kongwe)
Oda: Poales (Mimea kama manyasi)
Familia: Poaceae (Mimea iliyo na mnasaba na nyasi)
Jenasi: Triticum
L.
Spishi: T. aestivum L.

T. dicoccum Schrank
T. durum Desf.
T. monococcum L.
T. spelta L.

Ngano ni mmea wa familia ya manyasi katika ngeli ya monokotiledoni. Mbegu au punje za ngano ni nafaka ambayo ni chakula muhimu katika sehemu nyingi za dunia hasa kwenye kanda zisizo na joto au baridi kali.

Ngano ni kati ya nafaka muhimu zaidi zinazoliwa na watu pamoja na mhindi na mpunga. Ngano hutumiwa hasa kwa kuisaga kuwa unga. Unga wa ngano hutumiwa kwa mkate, chapati na pasta.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy