Nyuki

Nyuki
Jike la nyuki-bungu (Xylocopa caffra)
Jike la nyuki-bungu (Xylocopa caffra)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye mwili wenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Hymenoptera (Wadudu wenye mabawa mangavu)
Nusuoda: Apocrita (Hymenoptera wenye kiuno chembamba sana)
Familia ya juu: Apoidea
(bila tabaka): Anthophila (Nyuki)
Ngazi za chini

Familia 7:

Mwili wa nyuki. A: Kichwa B: Toraksi (kidari) C: Fumbatio. 1: Gena (shavu) 2: Verteksi (paji) 3: Oselli (macho sahili) 4: Papasio 5: Jicho tata 6: Ndevu 7: Kinywa 8: Mguu wa mbele 9: Femuri (paja) 10: Mguu wa kati 11: Ukucha 12: Tarsi 13: Tibia (goko) 14: Mguu wa nyuma 15: Sterno 16: Mwiba 17: Ubawa wa nyumba 18: Ubawa wa mbele

Nyuki ni wadudu wa kundi bila tabaka Anthophila katika familia ya juu Apoidea ya oda Hymenoptera wenye mabawa manne angavu na mwiba nyuma ya mwili wao. Hukusanya mbelewele na mbochi ya maua kama chakula chao.

Spishi inayojulikana hasa ni nyuki-asali (Apis mellifera) ambaye hufugwa kila mahali duniani. Kuna spishi zaidi ya 20,000 zinazojumlishwa na biolojia kati ya nyuki lakini ni wale wa jenasi Apis wanaotengeneza asali inayovunwa kwa matumizi ya binadamu.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy