Raila Odinga

Raila Amolo Odinga

Raila Odinga (alizaliwa 7 Januari 1945) ni mwanasiasa kutoka Kenya aliyehudumu kama Waziri mkuu kutoka mwaka wa 2008 hadi 2013. Anadhaniwa kuwa kiongozi wa upinzani nchini Kenya kuanzia 2013 kwani katiba mpya ya Kenya haina nafasi hii.

Alikuwa mbunge wa Langata kuanzia 1992 hadi 2007. Raila Odinga alihudumu kwenye baraza la mawaziri la Kenya kama waziri wa nishati kuanzia 2001 hadi 2002, na baadaye kama waziri wa barabara, kazi ya umma na makazi kuanzia 2003 hadi 2005. Odinga aliteuliwa kuwa mwakilishi wa juu wa maendeleo ya miundombinu katika Umoja wa Afrika mwaka wa 2018.

Ajulikana kote Kenya kwa jina lake la kwanza Raila, Rao au Baba. Watu wanaotoka kwenye kabila lake la waluo hupenda kumwita Agwambo, Tinga au Nyundo.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy